13 Ufalme wako ni ufalme wa milele,
mamlaka yako hudumu vizazi vyote.
Mwenyezi Mungu ni mwaminifu kwa ahadi zake zote
na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya.
14 Mwenyezi Mungu huwategemeza wote waangukao,
na huwainua wote waliolemewa na mizigo yao.