22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu,
katika kusanyiko nitakusifu wewe.
23 Ninyi ambao mnamcha Mwenyezi Mungu, msifuni!
Ninyi nyote wazao wa Yakobo, mheshimuni yeye!
Mcheni yeye, ninyi wazao wa Israeli!
24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau
mateso ya aliyeteswa;
hakumficha uso wake
bali alisikiliza kilio chake.