3 Sauti ya Mwenyezi Mungu iko juu ya maji;
Mungu wa utukufu hupiga radi,
Mwenyezi Mungu hupiga radi juu ya maji makuu.
4 Sauti ya Mwenyezi Mungu ina nguvu;
sauti ya Mwenyezi Mungu ni tukufu.
5 Sauti ya Mwenyezi Mungu huvunja mierezi;
Mwenyezi Mungu huvunja vipande vipande
mierezi ya Lebanoni.