Pular para o conteúdo
Publicidade

Salmos 32

Furaha ya msamaha

1 Heri mtu aliyesamehewa makosa yake,

ambaye dhambi zake zimefunikwa.

2 Heri mtu yule ambaye Mwenyezi Mungu

hamhesabii dhambi,

na ambaye rohoni mwake

hamna udanganyifu.

3 Niliponyamaza, mifupa yangu ilichakaa

kwa kulia kwa maumivu makali mchana kutwa.

4 Usiku na mchana

mkono wako ulinilemea,

nguvu zangu zilinyonywa

kama vile katika joto la kiangazi.

5 Kisha nikakiri dhambi yangu kwako,

wala sikuficha uovu wangu.

Nilisema, "Nitaungama

makosa yangu kwa Mwenyezi Mungu."

Ndipo uliponisamehe

hatia ya dhambi yangu.

6 Kwa hiyo kila mtu mcha Mungu akuombe

wakati unapopatikana,

hakika maji makuu yatakapofurika

hayatamfikia yeye.

Veja também