Sifa na wema wa Mwenyezi Mungu
Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka.
1 Nitamtukuza Mwenyezi Mungu nyakati zote,
sifa zake zitakuwa mdomoni mwangu siku zote.
2 Nafsi yangu itajisifu katika Mwenyezi Mungu,
walioonewa watasikia na wafurahi.
3 Mtukuzeni Mwenyezi Mungu pamoja nami,
naam, na tulitukuze jina lake pamoja.