8 Onjeni mwone kwamba Mwenyezi Mungu ni mwema;
heri mtu yule anayemkimbilia.
9 Mcheni Mwenyezi Mungu enyi watakatifu wake,
kwa maana wale wamchao
hawapungukiwi na chochote.
10 Wana simba wenye nguvu
hutindikiwa na kuona njaa,
bali wale wanaomtafuta Mwenyezi Mungu
hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
11 Njooni, watoto wangu, mnisikilize,
nitawafundisha kumcha Mwenyezi Mungu.