3 Mtumaini Mwenyezi Mungu na utende yaliyo mema.
Kaa katika nchi ukafurahie malisho salama.
4 Jifurahishe katika Mwenyezi Mungu
naye atakupa haja za moyo wako.
5 Mkabidhi Mwenyezi Mungu njia yako,
mtumaini yeye, naye atatenda hili:
6 Yeye atafanya haki yako ing’ae kama mapambazuko,
na hukumu ya shauri lako kama jua la adhuhuri.