4 "Ee Mwenyezi Mungu, nijulishe mwisho wa maisha yangu
na hesabu ya siku zangu;
nijalie kujua jinsi maisha yangu
yanavyopita upesi.
5 Umefanya maisha yangu mafupi kama nyanda;
muda wangu wa kuishi ni kama
hauna thamani kwako.
Maisha ya kila mwanadamu
ni kama pumzi.
6 Hakika kila binadamu ni kama njozi
aendapo huku na huko:
hujishughulisha na mengi, lakini ni ubatili;
anakusanya mali nyingi,
wala hajui ni nani atakayejifaidi nayo.