Maombi ya mtu mgonjwa
1 Heri mtu yule anayemjali mnyonge,
Mwenyezi Mungu atamwokoa wakati wa shida.
2 Mwenyezi Mungu atamlinda na kuyahifadhi maisha yake,
atambariki katika nchi
na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
3 Mwenyezi Mungu atamtegemeza akiwa mgonjwa kitandani,
na atamwinua kutoka kitandani mwake.