4 Dhidi yako, wewe peke yako, nimetenda dhambi
na kufanya yaliyo mabaya machoni pako,
ili uthibitike kuwa wa kweli unaponena,
na kuwa na haki unapotoa hukumu.
5 Hakika mimi nilizaliwa mwenye dhambi,
mwenye dhambi tangu nilipotungwa mimba kwa mama yangu.
6 Hakika wewe wapendezwa na kweli inayotoka moyoni;
wanifundisha hekima ndani ya moyo wangu.
7 Nioshe kwa hisopo, nami nitakuwa safi,
unisafishe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
8 Unipe kusikia furaha na shangwe,
mifupa uliyoiponda na ifurahi.
9 Ufiche uso wako usizitazame dhambi zangu,
na uufute uovu wangu wote.