Kusifu na kushukuru
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo.
1 Ee Mungu, sifa zakungojea katika Sayuni;
kwako wewe nadhiri zetu zitatimizwa.
2 Ewe usikiaye maombi,
watu wote watakuja kwako wewe.
3 Tulipokuwa tumefunikwa kabisa na dhambi,
wewe ulisamehe makosa yetu.