Shukrani kwa Mwenyezi Mungu kwa ajili ya haki yake
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa muth-labeni. Zaburi ya Daudi.
1 Ee Mwenyezi Mungu, nitakutukuza kwa moyo wangu wote,
nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu.
2 Nitafurahi na kushangilia ndani yako.
Nitaliimbia sifa jina lako, Ewe Uliye Juu Sana.