Mwenyezi Mungu Mfalme mkuu
1 Mwimbieni Mwenyezi Mungu wimbo mpya;
mwimbieni Mwenyezi Mungu dunia yote.
2 Mwimbieni Mwenyezi Mungu, lisifuni jina lake;
tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
3 Tangazeni utukufu wake katika mataifa,
matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.