Mfalme amshukuru Mwenyezi Mungu kwa ushindi
1 Ahimidiwe Mwenyezi Mungu Mwamba wangu,
aifundishaye mikono yangu vita,
na vidole vyangu kupigana.
2 Yeye ni Mungu wangu wa upendo na ulinzi wangu,
ngome yangu na mwokozi wangu,
ngao yangu, ninayemkimbilia,
ambaye huwatiisha mataifa chini yangu.