Utukufu wa Mwenyezi Mungu katika uumbaji
1 Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu,
anga zahubiri kazi ya mikono yake.
2 Siku baada ya siku zinatoa habari,
usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
3 Hakuna msemo wala lugha,
ambapo sauti zao hazisikiki.
4 Sauti yao imeenea duniani pote,
nayo maneno yao yameenea
hadi miisho ya ulimwengu.
Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
5 linafanana na bwana arusi
akitoka chumbani mwake,
kama shujaa anavyofurahia
kukamilisha kushindana kwake.
6 Huchomoza upande mmoja wa mbingu,
na kufanya mzunguko wake
hadi upande mwingine.
Hakuna kilichojificha joto lake.
7 Torati ya Mwenyezi Mungu ni kamilifu,
ikihuisha nafsi.
Shuhuda za Mwenyezi Mungu ni za kuaminika,
zikimpa mjinga hekima.
8 Maagizo ya Mwenyezi Mungu ni kamili,
nayo hufurahisha moyo.
Amri za Mwenyezi Mungu huangaza,
zatia nuru machoni.