Ukuu na wema wa Mwenyezi Mungu
1 Mwimbieni Mwenyezi Mungu kwa furaha, enyi wenye haki;
wanyofu wa moyo wanapaswa kumsifu.
2 Msifuni Mwenyezi Mungu kwa kinubi,
mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
3 Mwimbieni wimbo mpya;
pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.