Pular para o conteúdo
Publicidade

Salmos 101

Ahadi ya mfalme juu ya uaminifu na haki

Ya Daudi. Zaburi.

1 Rehema na hukumu nitaziimba,

Ee BWANA, nitakuimbia zaburi.

2 1 Sam 18:14;Mwa 18:19;Kum 6:7;1 Fal 9:4 Nitakuwa na mwenendo usio na hatia;

Utakuja kwangu lini?

Nitakwenda kwa unyofu wa moyo

Ndani ya nyumba yangu.

3 Yos 23:6;1 Sam 12:20 Sitaweka mbele ya macho yangu

Neno la uovu.

Kazi yao waliopotoka naichukia,

Haitaambatana nami.

4 Mt 7:23;1 Kor 5:11;2 Tim 2:19 Moyo wa ukaidi utaondoka kwangu,

Lililo ovu sitalijua.

5 Mit 6:17;Lk 18:14 Amsingiziaye jirani yake kwa siri,

Huyo nitamwangamiza.

Mwenye macho ya kiburi na moyo wa majivuno,

Huyo sitamvumilia.

6 Rum 13:4 Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi,

Hao wakae nami.

Yeye aendaye katika njia kamilifu,

Ndiye atakayenitumikia.

7 Hatakaa ndani ya nyumba yangu

Mtu atendaye hila.

Asemaye uongo hatathibitika

Mbele ya macho yangu.

8 Yer 21:12;Hos 9:3 Kila asubuhi nitawaangamiza

Waovu wote nchini.

Nikiwatenga wote watendao uovu

Na mji wa BWANA.

Veja também