Publicidade

Salmos 113

Mungu msaidizi wa mhitaji

1 Haleluya.

Enyi watumishi wa BWANA, sifuni,

Lisifuni jina la BWANA.

2 Dan 2:20 Jina la BWANA lihimidiwe

Tangu leo na hata milele.

3 Isa 59:19;Hab 2:14;Mal 1:11;Ufu 11:15 Toka maawio ya jua hata machweo yake

Jina la BWANA husifiwa.

4 BWANA ni mkuu juu ya mataifa yote,

Na utukufu wake ni juu ya mbingu.

5 Ni nani aliye mfano wa BWANA,

Mungu wetu aketiye juu;

6 Isa 57:15 Anyenyekeaye kutazama,

Mbinguni na duniani?

7 1 Sam 2:8;Isa 26:19;Dan 12:2 Humwinua mnyonge kutoka mavumbini,

Na kumpandisha maskini kutoka jaani.

8 Ayu 36:7 Ili amketishe pamoja na wakuu,

Pamoja na wakuu wa watu wake.

9 1 Sam 2:5;Gal 4:27 Humweka nyumbani mwanamke aliye tasa,

Awe mama ya watoto mwenye furaha.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-