6 BWANA huwalinda wasio na hila;
Nilidhilika, akaniokoa.
7 Yer 6:16;Mt 11:29Ee nafsi yangu, urudi pumzikoni mwako,
Kwa kuwa BWANA amekutendea ukarimu.
8 Maana umeniponya nafsi yangu na mauti,
Macho yangu na machozi,
Na miguu yangu na kuanguka.
9 Nitaenenda mbele za BWANA
Katika nchi za walio hai.