Pular para o conteúdo
Publicidade

Salmos 118

Wimbo wa ushindi

1 1 Nya 16:18,34;2 Nya 5:13;7:3;Ezr 3:11;Zab 100:5;106:1;107:1;136:1;Yer 33:11 Haleluya.

Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema,

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

2 Zab 115:9 Israeli na aseme sasa,

Ya kwamba fadhili zake ni za milele.

3 Mlango wa Haruni na waseme sasa,

Ya kwamba fadhili zake ni za milele.

4 Wamchao BWANA na waseme sasa,

Ya kwamba fadhili zake ni za milele.

5 Zab 18:19 Katika shida yangu nilimwita BWANA;

BWANA akanijibu akaniweka panapo nafasi.

6 Ebr 13:6;Rum 8:31 BWANA yuko upande wangu, sitaogopa;

Mwanadamu atanitenda nini?

7 Zab 54:4 BWANA yuko upande wangu, msaidizi wangu,

Kwa hiyo nitawaona wanaonichukia wakiwa wameshindwa.

8 Zab 62:8;Isa 2:22;Yer 17:5,7 Ni heri kumkimbilia BWANA

Kuliko kuwatumainia wanadamu.

9 Zab 146:3;Isa 30:2,3 Ni heri kumkimbilia BWANA.

Kuliko kuwatumainia wakuu.

10 Mataifa yote walinizunguka;

Kwa jina la BWANA niliwakatilia mbali.

11 Zab 88:17 Walinizunguka, naam, walinizunguka;

Kwa jina la BWANA niliwakatilia mbali.

12 Kum 1:44;Mhu 7:6 Walinizunguka kama nyuki,

Walizimika kama moto wa miibani;

Kwa jina la BWANA niliwakatilia mbali.

13 Ulinisukuma sana ili nianguke;

Lakini BWANA akanisaidia.

14 Kut 15:2;Isa 12:2 BWANA ni nguvu zangu na wimbo wangu,

Naye amekuwa wokovu wangu.

15 Sauti ya furaha na wokovu

Imo hemani mwao wenye haki;

Mkono wa kulia wa BWANA hutenda makuu.

16 Kut 15:6 Mkono wa kulia wa BWANA umetukuzwa;

Mkono wa kulia wa BWANA hutenda makuu.

17 Zab 6:5;73:28 Sitakufa bali nitaishi,

Nami nitayasimulia matendo ya BWANA.

18 Mit 3:11,12;1 Kor 11:32 BWANA ameniadhibu sana,

Lakini hakuniacha nife.

19 Isa 26:2 Nifungulieni malango ya haki,

Nitaingia na kumshukuru BWANA.

20 Zab 24:7;Isa 35:8 Lango hili ni la BWANA,

Wenye haki ndio watakaoliingia.

21 Nitakushukuru kwa maana umenijibu,

Nawe umekuwa wokovu wangu.

22 Mt 21:42;Mk 12:10;Lk 20:17;Mdo 4:11;Efe 2:20;1 Pet 2:4,7 Jiwe walilolikataa waashi

Limekuwa jiwe kuu la pembeni.Mt 21:42;Mk 12:10-11

23 Ayu 5:9 Neno hili limetoka kwa BWANA,

Nalo ni ajabu machoni petu.

24 2 Kor 6:2 Siku hii ndiyo aliyoifanya BWANA,

Tutashangilia na kuifurahia.

25 Mt 21:9;Mk 11:9;Yn 12:13 Ee BWANA, utuokoe, twakusihi;

Ee BWANA, utufanikishe, twakusihi.

26 Zek 4:7;Mt 21:9;23:39;Mk 11:9;Lk 13:35;19:38;Yn 12:13 Na abarikiwe yeye ajaye kwa jina la BWANA;

Tumewabariki toka nyumbani mwa BWANA.

27 Est 8:16;Mik 7:9;Mal 4:2 BWANA ndiye aliye Mungu,

Naye ndiye aliyetupa nuru.

Ifungeni dhabihu kwa kamba

Pembeni mwa madhabahu.

28 Kut 15:2;Isa 25:1 Ndiwe Mungu wangu, nami nitakushukuru,

Ndiwe Mungu wangu, nami nitakutukuza.

29 Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema,

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

Veja também