* * *
9 Mit 1:4,10Jinsi gani kijana aisafishe njia yake?
Kwa kutii, akilifuata neno lako.
10 2 Nya 15:15Kwa moyo wangu wote nimekutafuta,
Usiniache nipotee mbali na maagizo yako.
11 Lk 2:19Moyoni mwangu nimeliweka neno lako,
Nisije nikakutenda dhambi.
12 Ee BWANA, umehimidiwa,
Unifundishe amri zako.
13 Kwa midomo yangu nimezisimulia
Hukumu zote za kinywa chako.
14 Nimeifurahia njia ya shuhuda zako
Kana kwamba ni mali mengi.
15 Zab 1:2Nitayatafakari maagizo yako,
Na kuziangalia njia zako.
16 Nitajifurahisha sana kwa amri zako,
Sitalisahau neno lako.