Wimbo wa kupanda mlima.
1 Omb 3:55;Yon 2:2 Ee BWANA, toka vilindini nimekulilia.
2 Bwana, uisikie sauti yangu.
Masikio yako na yaisikilize
Sauti ya dua zangu.
3 Zab 143:2;Yn 8:7-9;Rum 3:20 BWANA, kama Wewe ungehesabu maovu,
Ee Bwana, nani angesimama?
4 2 The 1:6;Zab 37:2;Yer 17:6;Kut 3:4-7;Efe 1:7;1 Fal 8:40;Yer 33:8,9;Ebr 12:28 Lakini kwako kuna msamaha,
Ili Wewe uogopwe.
5 Isa 26:8 Nimemngoja BWANA, roho yangu imengoja,
Na neno lake nimelitumainia.
6 Nafsi yangu inamngoja Bwana,
Kuliko walinzi waingojavyo asubuhi,
Naam, walinzi waingojao asubuhi.
7 Isa 55:7 Ee Israeli, umtarajie BWANA;
Maana kwa BWANA kuna fadhili,
Na kwake kuna ukombozi mwingi.
8 Mt 1:21;Tit 2:14 Yeye atamkomboa Israeli na maovu yake yote.