1 1 Nya 16:34;2 Nya 5:13;7:3;Ezr 3:11;Zab 100:5;106:1;107:1;118:1;Yer 33:11 Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
2 Kut 18:11;Kum 10:17 Mshukuruni Mungu wa miungu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
3 1 Tim 6:15;Ufu 17:14 Mshukuruni Bwana wa mabwana;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
4 Yeye peke yake afanya maajabu makuu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
5 Mwa 1:1;Mit 3:19 Yeye aliyeumba mbingu kwa fahamu zake;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
6 Mwa 1:2;Yer 10:12 Yeye aliyeitandaza nchi juu ya maji;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
7 Mwa 1:16;Kum 4:19 Yeye aliyeumba mianga mikubwa;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
8 Jua litawale mchana;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
9 Mwezi na nyota zitawale usiku;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
10 Kut 12:29 Yeye aliyewapiga Wamisri kwa kuwaua wazaliwa wao wa kwanza;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
11 Kut 12:51 Akawatoa Waisraeli katikati yao;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
12 Kwa mkono hodari na mkono ulionyoshwa;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
13 Zab 78:13;Kut 14:21-29 Yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
14 Akawavusha Israeli katikati yake;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
15 Akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
16 Kum 8:15 Yeye aliyewaongoza watu wake jangwani;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
17 Yeye aliyewapiga wafalme wakuu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
18 Kum 29:7 Akawaua wafalme mashuhuri;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
19 Hes 21:21-30 Sihoni, mfalme wa Waamori;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
20 Hes 21:31-35 Na Ogu, mfalme wa Bashani;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
21 Yos 12:1 Akaitoa nchi yao iwe urithi;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
22 Urithi wa Israeli mtumishi wake;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
23 Mwa 8:1;Kum 32:36;Zab 102:17;Isa 63:9;Lk 1:48 Aliyetukumbuka katika unyonge wetu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
24 Akatuokoa na watesi wetu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
25 Zab 104:27 Yeye akipaye kila kiumbe chakula chake;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
26 Mshukuruni Mungu wa mbingu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.