Pular para o conteúdo
Publicidade

Zaburi 141

Sala ya kutaka kulindwa kutoka kwenye uovu

1 Ee BWANA, nimekuita, unijie hima,

Uisikie sauti yangu nikuitapo.

2 Efe 5:2;1 Tim 2:8;Ufu 5:8 Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba,

Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni.

3 Ee BWANA, uweke mlinzi kinywani pangu,

Mngojezi mlangoni pa midomo yangu.

4 Mt 6:14;20:15;Mit 23:6 Usiuelekeze moyo wangu kunako jambo baya,

Nisiyazoelee matendo yasiyofaa,

Pamoja na watu watendao maovu;

Wala nisile vyakula vyao vya anasa.

5 Mwenye haki na anipige, itakuwa fadhili;

Anikemee, itakuwa kama mafuta kichwani;

Kichwa changu kisikatae,

Maana siachi kusali kati ya mabaya yao.

6 Wakuu wao wakiangushwa kando ya genge,

Watayasikia maneno yangu, maana ni matamu.

7 2 Kor 1:9 Kama kupasua kuni na kuzichanja juu ya nchi,

Ndivyo ilivyo mifupa yetu mdomoni pa kuzimu.

8 Zab 25:15 Macho yangu yanakuelekea Wewe, MUNGU Bwana,

Nimekukimbilia Wewe, usiniache bila kinga.

9 Unilinde kutoka kwa mtego walionitegea,

Na kutoka kwa matanzi ya watendao maovu.

10 Est 7:10;Zab 7:15 Wabaya na waanguke katika nyavu zao wenyewe,

Wakati ninapopita salama.

Veja também