Publicidade

Salmos 15

Nani atakaa katika patakatifu pa Mungu?

Zaburi ya Daudi.

1 Zab 2:5 BWANA, ni nani atakayekaa

Katika hema yako?

Ni nani atakayeishi

Katika kilima chako kitakatifu?

2 Zab 84:11;Isa 33:15,16 Ni mtu aendaye kwa ukamilifu,

Na kutenda haki.

Asemaye kweli kwa moyo wake,

3 Asiyesingizia kwa ulimi wake.

Wala kumtenda mwenziwe mabaya,

Wala kumsengenya jirani yake.

4 Yos 9:18-20 Anayedharau waovu Machoni pake,

Bali huwaheshimu wamchao BWANA

Aliyeapa ingawa kwa hasara yake,

Hayabadili maneno yake.

5 Eze 18:8,9 Asiyetoa fedha yake apate kula riba,

Asiyepokea rushwa amwangamize asiye na hatia.

Mtu atendaye mambo hayo

Hataondoshwa milele.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-