Publicidade

Salmos 16

Wimbo wa imani na usalama kwa Mungu

Wimbo wa Daudi.

1 Zab 25:20 Mungu, unihifadhi mimi,

Kwa maana nakukimbilia Wewe.

2 Nimemwambia BWANA, Ndiwe BWANA wangu;

Sina wema ila utokao kwako.

3 Nao watakatifu waliopo duniani, ndio Walio bora,

Hao ndio niliopendezwa nao.

4 Huzuni zao zitaongezeka

Wambadilio Mungu kwa mwingine;

Sitazimimina sadaka zao za damu,

Wala kuyataja majina yao midomoni mwangu.

5 BWANA ndiye fungu la posho langu,

Na la kikombe changu;

Wewe unayaamua maisha yangu.

6 Mipaka yangu imeangukia mahali pema,

Naam, nimepata urithi mzuri.

7 Nitamhimidi BWANA aniongozaye,

Wakati wa usiku pia moyo wangu hunishauri.

8 Mdo 2:25-28 Nimemweka BWANA mbele yangu daima,

Kwa kuwa yuko kuliani mwangu, sitaondoshwa.

9 Kwa hiyo moyo wangu unafurahi,

Nayo nafsi yangu inashangilia,

Naam, mwili wangu nao utakaa kwa kutumaini.

10 Mdo 13:35;Zab 49:15;Mdo 2:27;Dan 9:24;Lk 1:35 Maana hutaitupa kuzimu nafsi yangu,

Wala hutamtoa mtakatifu wako aone uharibifu.

11 Mdo 2:28 Utanijulisha njia ya uzima;

Mbele za uso wako kuna furaha tele;

Na katika mkono wako wa kulia

Mna mema ya milele.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-