Shukrani za kifalme kwa ushindi
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa BWANA, aliyomwambia BWANA wakati BWANA alipomwokoa kutoka kwa mkono wa adui zake wote na kutoka kwa mkono wa Sauli. Akasema:
1 Wewe, BWANA, nguvu yangu, nakupenda sana;
2 BWANA ni jabali langu, na boma langu, na mwokozi wangu,
Mungu wangu, mwamba wangu ninayemkimbilia,
Ngao yangu, na pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu.
3 Namwita BWANA astahiliye kusifiwa,
Hivyo nitaokoka na adui zangu.