Pular para o conteúdo
Publicidade

Salmos 19

Utukufu wa Mungu katika viumbe na hukumu

1 Isa 40:22;Rum 1:19Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu,

Na anga laitangaza kazi ya mikono yake.

2 Mchana husemezana na mchana,

Usiku hutolea usiku maarifa.

3 Hakuna usemi wala maneno,

Sauti yao haisikilikani.

4 Rum 10:18Sauti yao imeenea duniani kote,

Na maneno yao hadi miisho ya ulimwengu.

Katika hizo ameliwekea jua hema,

5 Mhu 11:7Nalo hutokeza kama bwana arusi akitoka chumbani mwake,

Lafurahi kama mtu aliye hodari

Kwenda mbio katika njia yake.

6 Mhu 1:5Kuchomoza kwake ni katika mwisho wa mbingu,

Na kuzunguka kwake ni hadi miisho ya mbingu,

Wala hakuna kitu

Kisichofikiwa na joto lake.

7 Sheria ya BWANA ni kamilifu,

Huiburudisha nafsi.

Ushuhuda wa BWANA ni amini,

Humtia hekima mtu asiye nayo.

8 Neh 9:13;Rum 7:12Maagizo ya BWANA ni ya adili,

Huufurahisha moyo.

Amri ya BWANA ni safi,

Huyatia macho nuru.

Veja também