9 Kicho cha BWANA ni kitakatifu,
Kinadumu milele.
Hukumu za BWANA ni kweli,
Zina haki kabisa.
10 Ni za kutamanika kuliko dhahabu,
Kuliko wingi wa dhahabu safi.
Nazo ni tamu kuliko asali,
Kuliko sega la asali.
11 Tena mtumishi wako huonywa kwazo,
Katika kuzishika kuna thawabu kuu.