Publicidade

Salmos 20

Sala ya ushindi

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 Isa 50:10 BWANA akujibu siku ya dhiki,

Jina la Mungu wa Yakobo likuinue.

2 Akutumie msaada toka patakatifu pake,

Na kukutegemeza toka Sayuni.

3 Azikumbuke sadaka zako zote,

Na kuzitakabali dhabihu zako.

4 1 Yoh 5:14,15 Akujalie kwa kadiri ya haja ya moyo wako,

Na kukutimizia mipango yako yote.

5 Isa 12:1,2;1 Sam 17:45 Na tuushangilie wokovu wako,

Kwa jina la Mungu wetu tuzitweke bendera zetu.

BWANA akutimizie matakwa yako yote.

6 Sasa najua kuwa BWANA amwokoa masihi20:6 Au, mtiwa mafuta. wake;

Atamjibu toka mbingu zake takatifu,

Kwa matendo makuu ya wokovu

Ya mkono wake wa kulia.

7 Amu 7:7 Hawa wanataja magari na hawa farasi,

Lakini sisi tutalitaja jina la BWANA, Mungu wetu.

8 Wao wameinama na kuanguka,

Bali sisi tumeinuka na kusimama.

9 BWANA, umwokoe mfalme,

Utuitikie siku tuitayo.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-