6 Sasa najua kuwa BWANA amwokoa masihi wake;
Atamjibu toka mbingu zake takatifu,
Kwa matendo makuu ya wokovu
Ya mkono wake wa kulia.
7 Hawa wanataja magari na hawa farasi,
Lakini sisi tutalitaja jina la BWANA, Mungu wetu.
8 Wao wameinama na kuanguka,
Bali sisi tumeinuka na kusimama.