7 Zab 91:2Kwa kuwa mfalme humtumainia BWANA,
Na kwa fadhili zake Aliye Juu hatatikisika.
8 Mkono wako utawapata adui zako wote,
Mkono wako wa kulia utawapata wanaokuchukia.
9 Kum 32:22Utawafanya kuwa kama tanuri ya moto,
Wakati wa ghadhabu yako.
BWANA atawameza kwa ghadhabu yake,
Na moto utawateketeza.