22 Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu,
Katikati ya kusanyiko nitakusifu.
23 Ninyi mnaomcha BWANA, msifuni,
Enyi nyote mlio wazawa wa Yakobo, mtukuzeni,
Mcheni, enyi nyote mlio wazawa wa Israeli.
24 Maana hapuuzi
Wala kuchukizwa na mateso ya anayeteswa,
Wala hamfichi uso wake,
Bali humsikia akimlilia.