Publicidade

Salmos 27

Wimbo wa ushindi katika Bwana wa Daudi

Ya Daudi.

1 BWANA ni nuru yangu na wokovu wangu,

Nimwogope nani?

BWANA ni ngome ya uzima wangu,

Nimhofu nani?

2 Watenda mabaya waliponikaribia,

Wanile nyama yangu,

Watesi wangu na adui zangu,

Walijikwaa wakaanguka.

3 Jeshi lijapojipanga kupigana nami,

Moyo wangu hautaogopa.

Vita vijaponitokea,

Hata hapo nitatumainia BWANA.

4 Neno moja nimelitaka kwa BWANA,

Nalo ndilo nitakalolitafuta,

Nikae nyumbani mwa BWANA

Siku zote za maisha yangu,

Niutazame uzuri wa BWANA,

Na kutafakari hekaluni mwake.

5 Mit 18:10;Isa 4:6;Kol 3:3 Maana atanisitiri bandani mwake siku ya mabaya,

Atanisitiri katika sitara ya hema yake,

Na kuniinua juu ya mwamba.

6 Na sasa kichwa changu kitainuka

Juu ya adui zangu wanaonizunguka.

Nami nitatoa dhabihu za shangwe hemani mwake;

Nitaimba, naam, nitamhimidi BWANA.

7 Ee BWANA, usikie, kwa sauti yangu ninalia,

Unifadhili, unijibu.

8 Uliposema, "Nitafuteni uso wangu,"

Moyo wangu umekuambia,

BWANA, uso wako nitautafuta.

9 Usinifiche uso wako,

Usimkatalie mtumishi wako kwa hasira.

Umekuwa msaada wangu, usinitupe,

Wala usiniache, Ee Mungu wa wokovu wangu.

10 Isa 49:15;Yn 16:32;2 Tim 4:16-18 Hata baba yangu na mama yangu wakiniacha,

Bali BWANA atanikaribisha kwake.

11 Ee BWANA, unifundishe njia yako,

Na kuniongoza katika njia iliyonyoka;

Kwa sababu yao wanaoniotea;

12 1 Sam 22:9;Mt 26:59,60 Usinitie katika nia ya watesi wangu;

Maana mashahidi wa uongo wamenijia,

Nao watoao jeuri kama pumzi.

13 Zab 112:7,8 Naamini ya kuwa nitauona wema wa BWANA

Katika nchi ya walio hai.

14 Zab 62:1,5;Isa 25:9;Hab 2:3 Umtumainie BWANA, uwe imara,

Upige moyo konde, naam, umngoje BWANA.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_12-11-46-