Mwamini Mungu katika dhiki
1 2 Sam 15:13—17:22BWANA, watesi wangu wamezidi kuwa wengi,
Ni wengi wanaonishambulia,
2 2 Sam 16:8;Zab 22:7,8Ni wengi wanaoiambia nafsi yangu,
Hana wokovu huyu kwa Mungu.
3 2 Fal 25:27;Zab 27:6Lakini Wewe, BWANA, U ngao yangu pande zote,
Utukufu wangu na mwinua kichwa changu.
4 Kwa sauti yangu namwita BWANA
Naye aniitikia toka mlima wake mtakatifu.
5 Zab 4:8;Mit 3:24;Mdo 12:6Nilijilaza na kulala usingizi, kisha ninaamka tena,
Kwa kuwa BWANA ananitegemeza.
6 Sitayaogopa maelfu na maelfu ya watu,
Waliojipanga Juu yangu pande zote.