Publicidade

Salmos 30

Shukrani kwa kuponywa maradhi mabaya

Zaburi. Wimbo wa kuweka wakfu hekalu. Ya Daudi.

1 Ee BWANA, nitakutukuza kwa maana umeniinua,

Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu.

2 Zab 6:2-4 Ee BWANA, Mungu wangu,

Nilikulilia ukaniponya.

3 Zab 40:1,2 Umeniinua nafsi yangu,

Ee BWANA, kutoka kuzimu.

Umenihuisha na kunitoa

Miongoni mwao washukao Shimoni.

4 Mwimbieni BWANA zaburi,

Enyi watauwa wake.

Na kutoa shukrani.

Kwa kukumbuka utakatifu wake.

5 Zab 16:11;Ufu 22:17 Maana ghadhabu zake ni za muda mfupi tu;

Radhi yake ni ya milele.

Kilio huweza kuwapo usiku,

Lakini furaha huja asubuhi.

6 Ayu 29:18 Nami nilipofanikiwa nilisema,

Sitaondoshwa milele.

7 Zab 104:29 BWANA, kwa radhi yako

Wewe uliuimarisha mlima wangu.

Uliuficha uso wako,

Nami nikafadhaika.

8 Ee BWANA, nilikulilia Wewe,

Naam, kwa BWANA niliomba dua.

9 Zab 115:17 Mna faida gani katika damu yangu

Nishukapo Shimoni?

Mavumbi yatakusifu?

Yatautangaza uaminifu wako?

10 Zab 4:1 Ee BWANA, usikie, unirehemu,

BWANA, uwe msaidizi wangu.

11 2 Sam 6:14 Umegeuza msiba wangu kuwa ngoma;

Umeniondolea huzuni yangu, kunijalia furaha tele.

12 Ili nafsi yangu ikusifu,

Wala isinyamaze.

Ee BWANA, Mungu wangu,

Nitakushukuru milele.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-