Sala na sifa kwa kukombolewa kutoka kwa adui
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1 Nimekukimbilia Wewe, BWANA,
Nisiaibike milele.
Kwa haki yako uniponye,
2 Unitegee sikio lako, uniokoe hima.
Uwe kwangu mwamba wa nguvu,
Ngome thabiti ya kuniokoa.
3 Ndiwe mwamba wangu na ngome yangu;
Kwa ajili ya jina lako uniongoze na unichunge.
4 Utanitoa katika wavu walionitegea kwa siri,
Maana Wewe ndiwe ngome yangu.
5 Mikononi mwako naiweka roho yangu;
Umenikomboa, Ee BWANA, Mungu wa kweli.