Publicidade

Salmos 32

Shangwe kwa kusamehewa

Ya Daudi. Funzo

1 Rum 4:7-8;Zab 85:2 Heri aliyesamehewa dhambi,

Na kuondolewa makosa yake.

2 Law 17:4;Rum 5:13;Yn 1:47;2 Kor 1:12 Heri ambaye BWANA hamhesabii hatia,

Na ambaye rohoni mwake hamna hila.

3 Nilipokosa kuungama dhambi zangu, mifupa yangu ilipooza

Kwa kulia kwangu mchana kutwa.

4 Kwa maana mchana na usiku

Mkono wako ulinilemea.

Jasho langu likakauka hata nikawa

Kama nchi kavu wakati wa kaskazi.

5 Mit 28:13;Isa 65:24;Lk 15:18 Ndipo nikakuungamia dhambi yangu,

Wala sikuuficha upotovu wangu.

Nilisema, Nitayakiri maasi yangu kwa BWANA,

Nawe ukanisamehe upotovu wa dhambi yangu.

6 1 Tim 1:16;Isa 55:6;Yn 7:34 Kwa hiyo, hebu kila akuaminiye

Akuombe awapo katika dhiki.

Hakika maji makuu yafurikapo,

Hayatamfikia yeye.

7 Zab 9:9;Mit 18:10;Isa 4:6;Mt 23:37;Kol 3:3 Kimbilio langu utanilinda nisipate mateso,

Utanizungusha nyimbo za kufurahia wokovu wangu.

8 Isa 48:17 Nitakufundisha na kukuonesha njia utakayoiendea;

Nitakushauri, jicho langu likikutazama.

9 Msiwe kama farasi wala nyumbu,

Wasiokuwa na akili.

Kwa matandiko ya lijamu na hatamu

Sharti kuwazuia hao, au hawatakukaribia.

10 Mit 13:21;Zab 34:8;Mit 16:20;Yer 17:7 Naye mtu mwovu ana mapigo mengi,

Bali amtumainiaye BWANA fadhili zitamzunguka.

11 Mfurahieni BWANA;

Shangilieni, enyi wenye haki

Pigeni vigelegele vya furaha;

Ninyi nyote mlio wanyofu wa moyo.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-