11 Njoni, enyi wana, mnisikilize,
Nami nitawafundisha kumcha BWANA.
12 Ni nani atamaniye uzima na atakaye kuishi,
Siku nyingi afurahie mema?
13 Uuzuie ulimi wako na mabaya,
Na midomo yako na kusema hila.
14 Uache mabaya ukatende mema,
Utafute amani ukaifuatie.