8 1 Pet 2:3Onjeni muone ya kuwa BWANA yu mwema;
Heri mtu yule anayemtumainia.
9 Flp 4:19Mcheni BWANA, enyi watakatifu wake,
Maana, wamchao hawapungukiwi kitu.
10 Wanasimba hutindikiwa, na kuona njaa;
Bali wamtafutao BWANA hawapungukiwi kitu chochote kilicho chema.
11 Njoni, enyi wana, mnisikilize,
Nami nitawafundisha kumcha BWANA.