Pular para o conteúdo
Publicidade

Salmos 36

Uovu wa watu na wema wa Mungu

Kwa mwimbishaji. Ya Daudi, mtumishi wa Bwana

1 Rum 3:18;Mwa 20:11;Mit 8:13;Mhu 12:3 Kuasi kwake yule mwovu hunena moyoni mwake,

Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.

2 Kwa maana hujipendekeza machoni pake

Kuwa upotovu wake hautaonekana na kuchukiwa.

3 Yer 4:22 Maneno ya kinywa chake ni uovu na hila,

Ameacha kuwa na akili na kutenda mema.

4 Mik 2:1;Isa 65:2 Huwaza maovu kitandani pake,

Hujiweka katika njia mbaya; hauchukii ubaya.

5 Zab 57:10 Ee BWANA, fadhili zako zafika hata mbinguni,

Uaminifu wako hadi mawinguni.

6 Ayu 11:8;Rum 11:33;Ayu 7:20;Zab 145:9 Haki yako ni kama milima ya Mungu,

Hukumu zako ni vilindi vikuu,

Ee BWANA, unawalinda wanadamu na wanyama.

7 Rut 2:12 Ee Mungu, jinsi zilivyo na thamani fadhili zako!

Wanadamu huukimbilia uvuli wa mbawa zako.

8 Ayu 20:17;Ufu 22:1 Watashibishwa kwa unono wa nyumba yako,

Nawe utawanywesha kutoka mto wa furaha zako.

9 Isa 12:3;Yer 2:13;Zek 13:1;Yn 4:10,14;Ufu 21:6;Mdo 26:18;Efe 5:8;Kol 1:13;1 Pet 2:9 Maana kwako Wewe iko chemchemi ya uzima,

Katika nuru yako tutaona nuru.

10 Yer 22:16 Uwadumishie wakujuao fadhili zako,

Na wanyofu wa moyo uaminifu wako.

11 Mguu wa kiburi usinikaribie,

Wala mkono wa wasio haki usinifukuze.

12 Huko ndiko walikoanguka wafanyao maovu;

Wameangushwa chini wasiweze kusimama.

Veja também