Zaburi ya Daudi, kwa matoleo ya kumbukumbu.
1 Ee BWANA, usinilaumu katika ghadhabu yako,
Wala usiniadhibu kwa ukali wa hasira yako.
2 Kwa maana mishale yako imenichoma,
Na mkono wako umenipata.
3 Hamna uzima katika mwili wangu
Kwa sababu ya ghadhabu yako.
Wala hamna amani mifupani mwangu
Kwa sababu ya hatia zangu.
4 Maana dhambi zangu zimenifunika kichwa,
Kama mzigo mzito zimenilemea mno.
5 Majeraha yangu yananuka na kutunga usaha,
Kwa sababu ya upumbavu wangu.
6 Nimejipinda na kuinama sana,
Mchana kutwa ninaenda nikiomboleza.
7 Ayu 7:5 Maana viuno vyangu vimejaa homa,
Wala hamna uzima katika mwili wangu.
8 Nimedhoofika na kupondeka sana,
Nimeugua kwa fadhaa ya moyo wangu.
9 Bwana, haja zangu zote ziko mbele zako,
Kuugua kwangu hakukusitirika kwako.
10 Moyo wangu unadundadunda,
Nguvu zangu zimenitoka;
Nuru ya macho yangu nayo imeniondoka.
11 Lk 10:31 Wanipendao na rafiki zangu wanasimama mbali na pigo langu;
Na jamaa zangu wanasimama mbali.
12 Nao wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego;
Nao wanaotaka kunidhuru hunena mabaya;
Na kufikiri hila mchana kutwa.
13 Lakini kama kiziwi sisikii,
Nami ni kama bubu asiyefumbua kinywa chake.
14 Naam, nimekuwa kama mtu asiyesikia,
Ambaye hamna ubishi kinywani mwake.
15 Yer 14:8 Kwa kuwa nakungoja Wewe, BWANA,
Wewe utajibu, Ee Bwana, Mungu wangu.
16 Maana nilisema, Wasije wakanifurahia;
Wale wanaojitukuza juu yangu Mguu wangu unapoteleza.
17 Kwa maana mimi ni karibu na kusita,
Na maumivu yangu yako mbele yangu daima.
18 Ayu 31:33;Zab 32:5;Mit 28:13;2 Kor 7:9 Kwa maana nitaungama uovu wangu,
Na kusikitika kwa dhambi zangu.
19 Lakini walio adui zangu bila sababu wana nguvu,
Nao wanaonichukia bure wamekuwa wengi.
20 1 Yoh 3:12;1 Pet 3:13 Naam, wakilipa mabaya kwa mema,
Huwa adui zangu kwa kuwa nilifuata lililo jema.
21 Zab 22:1,11 Wewe, BWANA, usiniache,
Mungu wangu, usijitenge nami.
22 Kut 15:2;Isa 12:2 Ufanye haraka kunisaidia,
Ee Bwana, wokovu wangu.