Sala ya kutaka hekima na msamaha
Kwa mwimbishaji: kwa Yeduthuni. Zaburi ya Daudi.
1 1 Fal 2:4;Mit 4:26,27;Ebr 2:1;Kol 4:5 Nilisema, Nitazitunza njia zangu
Nisije nikakosa kwa ulimi wangu;
Nitajitia lijamu kinywani,
Maadamu mtu mbaya awapo mbele yangu.
2 Nilikuwa sisemi, nilinyamaa kimya,
Sina faraja, maumivu yangu yakazidi.
3 Yer 20:9 Moyo wangu ukawa moto ndani yangu,
Na katika kuwaza kwangu moto ukawaka;
Nilisema kwa ulimi wangu,
4 BWANA, unijulishe mwisho wangu,
Na idadi ya siku zangu ni ngapi;
Nijue jinsi maisha yangu yalivyo mafupi.
5 Zab 90:4 Tazama, umefanya siku zangu kuwa mashubiri;
Maisha yangu ni kama si kitu mbele zako.
Kila mwanadamu, ingawa amesitawi, ni ubatili.
6 Kweli, watu wote hupita kama kivuli;
Wao hujisumbua bure tu;
Wanajirundikia mali wala hawajui ni nani atakayeirithi.
7 Na sasa ninangoja nini, Ee Bwana?
Matumaini yangu ni kwako.
8 Uniokoe kutoka kwa maasi yangu yote,
Usinifanye niwe wa kulaumiwa na mpumbavu.
9 Nimenyamaza, sifumbui kinywa changu,
Maana Wewe ndiwe uliyeyafanya.
10 Uniondolee pigo lako;
Kwa mapigo ya mkono wako nimeangamia.
11 Ukimrudi mtu kwa kumkemea kwa uovu wake,
Watowesha uzuri wake kama nondo.
Kila mwanadamu ni ubatili.
12 Law 25:23;1 Nya 29:15 Ee BWANA, usikie maombi yangu,
Utege sikio lako niliapo,
Usiyapuuze machozi yangu.
Kwa maana mimi ni mgeni wako,
Msafiri kama baba zangu wote.
13 Ayu 10:20,21 Uache kunitazama, ndio nipate kufurahi tena,
Kabla sijafa na kutoweka kabisa.