Pular para o conteúdo
Publicidade

Salmos 46

Ulinzi wa Mungu kwa mji na watu wake

Kwa mwimbishaji. Ya Wakorahi. Kwa mtindo wa Alamothi. Wimbo.

1 Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu,

Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.

2 Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi,

Ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari.

3 Maji yake yajapovuma na kuumuka,

Ijapopepesuka milima kwa kiburi chake.

4 Isa 8:7;Ufu 22:1;2 Nya 6:6;Zab 48:1;Isa 60:14;Ebr 12:22 Kuna mto, vijito vyake vyaufurahisha mji wa Mungu,

Patakatifu pa maskani zake Aliye Juu.

5 Kum 23:14;Isa 12:6;Eze 43:7 Mungu yu katikati ya mji hautatetemeshwa;

Mungu atausaidia asubuhi na mapema.

6 Mataifa yanaghadhibika na falme kutetemeka;

Anatoa sauti yake, nchi inayeyuka.

7 BWANA wa majeshi yu pamoja nasi,

Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.

8 Njoni muyatazame matendo ya BWANA,

Jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.

9 Avikomesha vita hata mwisho wa dunia;

Avunja uta, akata mkuki, achoma moto magari.

10 Kut 14:13;Isa 2:11 Tulieni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu,

Nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi.

11 BWANA wa majeshi yu pamoja nasi,

Mungu wa Yakobo ni kimbilio46:11 Au ngome yetu. letu.

Veja também