Kwa mwimbishaji. Ya Wakorahi. Zaburi.
1 Enyi watu wote, pigeni makofi,
Mpigieni Mungu kelele kwa Sauti ya shangwe.
2 Kum 7:21;Neh 1:5;Mal 1:14 Kwa kuwa BWANA Aliye Juu, mwenye kuogofya,
Ndiye mfalme mkuu juu ya dunia yote.
3 Zab 18:47 Amewatiisha watu wa nchi chini yetu,
Na mataifa chini ya miguu yetu.
4 1 Pet 1:4 Ametuchagulia urithi wetu,
Fahari ya Yakobo ampendaye.
5 Zab 24:7-10;Mdo 1:9;Efe 4:8-10;1 Tim 3:16 Mungu amepaa kwa kelele za shangwe,
BWANA kwa sauti ya baragumu.
6 Mwimbieni Mungu sifa, imbeni sifa;
Imbeni sifa kwa mfalme wetu, imbeni sifa.
7 Zek 14:9;1 Kor 14:15 Maana Mungu ndiye mfalme wa dunia yote,
Imbeni kwa zaburi.
8 Mungu ayatawala mataifa,
Mungu ameketi katika kiti chake kitakatifu.
9 Wakuu wa watu wamekusanyika,
Kama watu wa Mungu wa Abrahamu.
Maana ngao za dunia zina Mungu,
Ametukuka sana.