4 Rum 3:4;Lk 15:21;Mwa 39:9Nimekutenda dhambi Wewe peke yako,
Na kufanya maovu mbele za macho yako.
Wewe ujulikane kuwa una haki unenapo,
Na kuwa safi utoapo hukumu.
5 Ayu 14:4;Yn 3:6;Rum 5:12Tazama, nikazaliwa nikiwa na hatia;
Mama yangu akanichukua mimba nikiwa na dhambi.
6 Tazama, wapendezwa na kweli iliyo moyoni;
Nawe utanifundisha hekima kwa siri,
7 Unisafishe kwa hisopo nami nitakuwa safi,
Unioshe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
8 Unifanye kusikia furaha na shangwe,
Mifupa uliyoiponda ifurahi.
9 Usitiri uso wako usitazame dhambi zangu;
Uzifute hatia zangu zote.