Publicidade

Salmos 52

Hukumu kwa waongo

Kwa mwimbishaji. Utenzi wa Daudi, wakati Doegi, Mwedomu alipomwendea Sauli na kumwambia, "Daudi ameingia nyumbani mwa Ahimeleki."

1 1 Sam 22:9-10;21:7 Kwa nini kujisifia uovu, Ewe jabari?

Wema wa Mungu upo sikuzote.

2 Zab 50:19;Mit 12:18;Zab 59:7 Ulimi wako watunga madhara,

Kama wembe mkali, Ewe mwenye hila.

3 Yer 9:4 Umependa mabaya kuliko mema,

Na uongo kuliko kusema kweli.

4 Umependa maneno yote ya kupoteza watu,

Ewe ulimi wenye hila.

5 Mit 2:22 Lakini Mungu atakuharibu hata milele;

Atakuondolea mbali;

Atakunyakua hemani mwako;

Atakung’oa katika nchi ya walio hai.

6 Ayu 22:19;Zab 58:10 Nao wenye haki wataona;

Wataingiwa na hofu na kumcheka;

7 Ayu 31:24,25;Zab 49:6 Kumbe! Huyu ndiye mtu yule,

Asiyemfanya Mungu kuwa kimbilio lake.

Aliutumainia wingi wa mali zake,

Na kufanya mali kimbilio lake.

8 Zab 92:13 Bali mimi ni kama mzeituni

Umeao katika nyumba ya Mungu.

Nazitumainia fadhili za Mungu milele na milele.

9 Zab 54:6 Nitakushukuru milele kwa maana umetenda;

Nitalingojea jina lako kwa kuwa ni jema;

Mbele ya wacha Mungu wako.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-