Kwa mwimbishaji: kwa ala za nyuzi za muziki. Utenzi wa Daudi, wakati Wazifu walipoenda na kumwambia Sauli, "Daudi amejificha kwetu".
1 Ee Mungu, kwa jina lako uniokoe,
Na kwa uweza wako unifanyie hukumu.
2 Ee Mungu, uyasikie maombi yangu,
Uyasikilize maneno ya kinywa changu.
3 Kwa maana wageni wamenishambulia;
Watu watishao wananitafuta nafsi yangu;
Hawakumweka Mungu mbele yao.
4 Zab 118:7;Isa 41:10;Rum 8:31,32;Ebr 13:6 Tazama, Mungu ndiye anayenisaidia;
Bwana ndiye anayenitegemeza nafsi yangu.
5 Zab 89:49 Atawarudishia adui zangu ubaya wao;
Uwaangamize kwa uaminifu wako.
6 Kwa ukunjufu wa moyo nitakutolea dhabihu;
Ee BWANA, nitalishukuru jina lako, maana ni jema.
7 Kwa kuwa limeniokoa na kila taabu;
Na jicho langu limeridhika
Kwa kuwatazama adui zangu.