Pular para o conteúdo
Publicidade

Salmos 57

Sifa na hakikisho katika mateso

Kwa mwimbishaji: kwa mtindo wa Usiharibu. Utenzi wa Daudi alipomponyoka Sauli na kujificha pangoni.

1 Isa 26:20 Unirehemu, Ee Mungu, unirehemu mimi,

Maana nafsi yangu imekukimbilia Wewe.

Nitaukimbilia uvuli wa mbawa zako,

Hadi misiba hii itakapopita.

2 Zab 138:8 Nitamwita MUNGU Aliye Juu,

Mungu anitimiziaye mambo yangu.

3 Zab 144:5;40:11 Atanitumia msaada toka mbinguni na kuniokoa,

Atawaaibisha wale wanaotaka kunishambulia.

Mungu atazituma

Fadhili zake na kweli yake.

4 Mit 30:14;Zab 64:3 Nafsi yangu i kati ya simba,

Nitastarehe kati yao waliowaka moto.

Wanadamu meno yao ni mikuki na mishale,

Na ndimi zao ni upanga mkali.

5 Zab 108:5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,

Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako.

6 Zab 9:15 Wameweka wavu ili kuninasa miguu;

Nimevunjika moyo;

Wamechimba shimo njiani mwangu;

Lakini wao wenyewe wametumbukia humo!

7 Zab 108:1 Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti,

Moyo wangu ni thabiti.

Nitaimba, nitaimba kwa sauti nzuri,

8 Amu 5:12 Amka, ee moyo wangu.

Amka, kinanda na kinubi,

Nitaamka alfajiri.

9 Ee Bwana, nitakushukuru kati ya watu,

Nitakuimbia sifa kati ya mataifa.

10 Zab 108:4 Maana fadhili zako ni kubwa hata mbinguni,

Na uaminifu wako hata mawinguni.

11 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,

Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako.

Veja também