Shukrani kwa mavuno mengi
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo.
1 Ee Mungu, wastahili sifa katika Sayuni,
Na kwako Wewe itaondolewa nadhiri.
2 Wewe usikiaye maombi,
Wote wenye mwili watakujia.
3 Tutakapozidiwa na matendo maovu
Wewe utatuondolea uovu wetu.